Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Makonda amesema mwanamke yeyote atakayeshushiwa kipigo na mwanaume, kuanzia sasa atoe taarifa kupitia simu ya mkononi namba 0682009009 ili mwanaume alietenda ukatili huo, atafutwe popote alipo na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Aidha Makonda amepanga kuliomba Bunge la Tanzania, linapofanya mabadiliko ya sheria ya ndoa, kiongezwe kipengele cha kukata asilimia 40 ya mshahara wa mwanaume, apatiwe mwanamke ambaye anajishughulisha na kazi za nyumbani, ili ikifika mwishoni mwa mwaka kila mmoja awe na cha kwake.
