Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mlinzi wa Meja Jenerali Mstaafu akamatwa

Jumatano , 13th Sep , 2017

Jeshi la Polisi linamshikilia mlinzi wa Meja Jenerali Mstaafu Vicent Mirataba na mfanyakazi mmoja wa benki kwa kuhusika kwa namna moja ama nyingine katika kupanga njama za shambulizi la Meja huyo lililotokea nyumbani kwake Ununio siku za hivi karibun

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar, Lazaro Mambosasa.

Hayo yameelezwa na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP), Lazaro Mambosasa wakati alipokuwa anaongea na waandishi wa habari na kusema kwa mujibu wa muhusika amewaeleza kwamba majira ya mchana huwa analinda peke yake lindo hilo huku akiwa na silaha aina ya shortgun.

"Katika mazingira ya kushangaza mlinzi huyo aliweka silaha kinyume kabisa na maadili ya utunzanji wa silaha maana aliiweka juu ya kitanda, halafu akatoka mikono mitupu kwenda kuwapa ushirikiano waliyofanya uhalifu huo kwa kuwafungulia mlango na kutenda uhalifu", amesema Mambosasa.

Pamoja na hayo, Kamanda Mambosasa ameendelea kwa kusema "Alitueleza kwamba aliamriwa akimbie naye akatii bila ya shuruti lakini silaha yake akaiacha pale pale alipokuwa ameiacha awali na kurudi baadae, askari huyu ambaye tuna uhakika amepitia mafunzo ya JKT angekuwa askari kweli wa kuhakikisha usalama wa maeneo anayoyalinda asingeenda kufungua geti bila ya kuwa na silaha. Kwa hiyo mashaka hayo ya msingi yametufanya tumkamate kwa kuwa aliiacha silaha na kutopigwa kofi au kwenzi na hao wahalifu".

Kwa upande mwingine, Kamanda Mambosasa amesema wamemkamata mmoja wa wafanyakazi wa benki ambaye anadai alikuwa anawasiliana na mtu wa nje ya ofisi ili aweze kumfuatilia Meja Jenerali Vicent wakati alipotoka kuchukua fedha benki.

HABARI ZAIDI

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani