Alhamisi , 13th Jan , 2022

Mhadhiri wa Chuo Kikuu kimoja nchini Morocco aliyekuwa anatuhumiwa kufaulisha wanafunzi wa kike kwa kufanya nao ngono amehukumiwa kifungo cha jela miaka miwili.

Picha

Hukumu hiyo ni ya kwanza kutolewa nchini Morocco kwa mtumishi mwandamizi wa kada hiyo kwenye vyuo vikuu vya Morocco.

Mhadhiri huyo wa uchumi katika Chuo Kikuu cha Hassan, kilichopo karibu na Casablanca, alitiwa hatiani kwa tabia chafu pamoja na makosa mengine.

Wahadhiri wengine wanne wanafikisha mahakamani hii leo kuhusiana na kashfa hiyo ya ufaulu kwa kutoa ngono.

Kesi hiyo iliibuliwa na chombo cha habari cha Morocco mwaka jana baada ya waandishi wake kunasa meseji za mapenzi baina ya wanafunzi na wahadhiri.