
Gari ambalo limekutwa na mwili wa mfanyabishara Muksini
Wakizungumza katika tukio hilo, baadhi ya mashuhuda wamesema majira ya saa 2:00 asubuhi wamelikuta gari hilo likiwa kandokando mwa barabara huku mwili huo ukiwa ndani ya gari.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa, amekiri kutokea kwa tukio hilo huku akisema bado uchunguzi unaendelea kufanyika ili kubaini chanzo cha tukio hilo.