Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbunge na mkewe watema madini ya Valentine's Day

Jumanne , 14th Feb , 2017

Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu akiwa ameambatana na mke wake Bi. Anna Jacob hii leo wametema madini kama fundisho kwa wanandoa, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya 'Siku ya Wapendanao' (Valentine's Day), tarehe 14 Februari kila mwaka.

Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu na Mkewe Bi. Anna Jacob

Wawili hao wamefunguka mengi kuhusu mahusiano yao, walipoambatana pamoja katika kipindi East Africa Breakfast cha EA Radio kinachoruka saa 11:00 alfajiri hadi saa 3:00 Asubuhi.

Huku wakionesha jinsi wanavyopendana, wawili hao wamesimulia jinsi walivyokutana, ambapo wamesema kuwa walikutana kwenye msiba, na kila mmoja akatokea kumpenda mwenzake bila kujali hali zao za kimaisha, takriba miaka 9 iliyopita.

Anna ametoa ujumbe kwa mabinti ambao hawajaolewa kwa kumesema katika mapenzi, haitakiwi mwanamke kumpenda mwanaume kwa sababu ya mali na ndiyo maana yeye alimpenda Kingu wakati huo hajawa mbunge, huku akibainisha kuwa alilazimika kubadili dini, ili wawe pamoja.

Pia Bi. Anna ambaye kitaaluma ni mtaalam wa masuala ya benki (Banker) amesisitiza suala la uaminifu katika ndoa, akiwataka watu wote walio katika ndoa watambue kuwa kilichowaunganisha ni uaminifu, hivyo hawapaswi kuvunja kiapo hicho huku akiweka wazi kuwa kosa pekee ambalo hawezi kulisamehe kwa mume wake ni la kuvunja uaminifu.

Akizungumzia ratiba za mume wake kama Mbunge, amesema kuwa hazimkwazi na tayari anazifahamu, na kwamba hata wakati anafikia kugombea ubunge alimshirikisha, na yeye alimpa sapoti ya kutosha.

Kwa upande wake Kingu, ameshauri wanandoa kuwa na uwazi katika kila jambo ikiwa ni pamoja na mali pamoja na kipato cha kila mmoja, huku akitupia lawama wanaume wengi ambao huwa na tabia ya kuwaficha wake zao baadhi ya mambo kuwa ni hatari na ni sababu ya ndoa nyingi kuvunjika, pamoja na wanaume wengi kufariki kwa shinikizo la daumu na kuacha wanawake wengi wakiwa wajane

Pia Kingu amewasihi wanandoa kuwa na moyo wa kuvumiliana na kuchukuliana mapungufu ili kulinda ndoa, ambapo ametolea mfano jinsi mke wake alivyombadilisha kutoka kuwa na tabia ya hasira za haraka hadi hakuwa mtulivu, na sasa anajigamba kuwa ni baba bora kutokana na aina ya mke aliyempata.

Sikiliza hapa Mazungumzo yalivyokuwa ndani ya Studio za EA Radio, katika kipindi cha EA Breakfast kinachoongozwa na Irene Tillya, Shaaban Lupa na Songa wa Songa.................................

HABARI ZAIDI

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani