
Mwenyekiti wa CHADEMA anayemaliza muda wake Freeman Mbowe.
Katika Uchaguzi huo nafasi ya Uenyekiti inawaniwa na wabunge wawili ambao ni Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe pamoja na Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe.
Katika nafasi ya makamu Mwenyekiti, inawaniwa na aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, huku Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea,akitangaza kujiondoa jana kwa kile alichokisema Tundu Lissu ndiye anafaa zaidi.
Jana Disemba 16, 2019, kwenye Mkutano na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Mawasiliano Itifaki na Mambo ya Nje (CHADEMA), John Mrema alisema majina ya wagombea wote yanapelekwa leo katika kikao Cha Baraza Kuu kwa
#HABARI Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema leo Disemba 16, 2019 ndiyo kimepokea rasmi barua ya kujiuzulu kwa uanachama wa Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye.
Aidha kimeeleza kujitoa kwa Mbunge Saed Kubenea, katika kuwania Umakamu Mwenyekiti wa chama hicho. pic.twitter.com/eLFPDAWleG
— East Africa Radio (@earadiofm) December 16, 2019