Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Matumizi ya gongo Rombo yapungua kwa 92% - DC

Jumanne , 30th Jun , 2015

Unywaji wa pombe haramu ya gongo na ambazo hazina viwango umepungua kwa asilimiaa 92 wilayani Rombo baada ya serikali kukamata zana mbalimbali zinazotumika kutengezea pombe hiyo

Baadhi ya wanawake wa wilaya ya Rombo wakiandamana kuelekea kwa mkuu wa wilaya kama ishara ya kuunga mkono juhudi za serikali kupambana na matumizi ya gongo

Unywaji wa pombe haramu ya gongo na ambazo hazina viwango umepungua kwa asilimiaa 92 wilayani Rombo baada ya serikali kukamata mitambo 178, mapipa 3,500 ya malighafi, lita 550 za gongo, lita 108,000 za sumu za viwanda vya wazalishaji wakubwa wa pombe hizo kwa miezi mitatu iuliyopita.

Mkuu wa wilaya ya Rombo Lembrise Kipuyo ametoa taarifa hiyo kwa mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo aliyepokea matembezi ya amani ya kuunga mkono juhudi za serikali za kupambana na upikaji na unywaji wa pombe hizo ambao unaathiri nguvu kazi yaliyoandaliwa na wanawake wa wilaya ya rombo...

Hata hivyo bw kipuyo ambaye anaongoza mapambano hayo baada ya kuhamia wilaya hiyo amesema, matembezi hayo yamempa nguvu na kasi mpya ya kupambana na wapikaji wakubwa wa pombe hizo ambao 58 kati yao wamekamatwa na kesi zao zinazoendelea mahakamani na wengine wamefungwa.

Katika taarifa yao wanawake hao wamewalaani baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanaohamasisha unywaji na upikaji wa pombe hizo kwa kuiomba serikali ihalalishe gongo na kumtaka mkuu huyo wa wilaya asikatishwe tamaa na viongozi wa aina hiyo ambao ni wapinzani wa maendeleo.

Akipokea matembezi hayo ya kilomita mbili mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Wilbard Ringia amewataka wananchi wa wilaya hiyo kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali ili kurejesha heshima ya kujieletea maendeleo kwa kufanya kazi kwa bidii ambayo imetoweka kutokana na unywaji wa pombe hizo.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea