Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Matatizo ya wanafunzi wa bweni yatatuliwa

Jumapili , 18th Aug , 2019

Jumla ya wasichana 170 katika shule ya Sekondari Tura iliyopo Uyui Tabora,  wamepata taulo za kike watakazotumia kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Makabidhiano ya taulo za kike katika Shule ya Sekondari ya Tura

Shule hiyo iliyopo zaidi ya kilometa 150 kutoka Tabora mjini ni shule ya Bweni kwa wasichana ambapo Mkuu wa shule hiyo Adam Shaban Mangao, ameeleza kuwa taulo hizo zitasaidia kupunguza matatizo kwa wanafunzi wawapo bwenini.

''Kampeni ya Namthamini itatatua tatizo wanafunzi kubaki bwenini na kukosa masomo maana ndio tatizo ambalo limekuwa likisababisha kupunguza ufaulu kutokana na watoto hawa kulazimika kukosa vipindi wanapokuwa kwenye hedhi lakini hawajatumiwa fedha za kujikimu na kuweza kununua taulo hizi'', amesema.

Aidha Mwalimu Mangao, amezipongeza na kuzishukuru East Africa Television na East East Africa Radio kwa kuichagua shule ya Tura, kuwa miongoni mwa shule nyingi zitakazofikiwa na Kampeni ya Namthamini mwaka huu.

Zoezi la ugawaji wa taulo za kike katika shule 4 za mkoani Tabora lilikamilika Jumamosi Agosti 17, 2019, ambapo zaidi ya wanafunzi 500 wamepata taulo za kike kwa mwaka mzima.

Shule nyingine zilizofikiwa katika mkoa huo ni pamoja na Ikomwa, Ndono pamoja na Idete, ambapo timu ya East Africa Television na East Africa Radio iliambatana na mkuu wa mkoa huo Aggrey Mwanri.

Katika mwaka wake wa tatu, Namthamini imefanikiwa kufika katika mikoa ya Manyara, Arusha na Tabora huku ikitarajiwa kufika katika mikoa mingine ikiwemo Dodoma.

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji