Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mapato ya maji taka na maji safi yaongezeka

Jumatatu , 8th Mar , 2021

Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi amesema kuwa utekelezaji wa miradi ya maji na usimamizi wake umeleta mafanikio kwa huduma ya maji nchini.

Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi

Dkt. Hassan Abbasi amebainisha hilo leo Machi 8, 2021 alipozungumza na vyombo vya habari ambapo amesema ubora wa huduma za maji nchini umeongezeka kutoka wastani wa 47% kwa vijijini na wastani wa 74% kwa miji mikuu.

Sambamba na ubora huo Dkt. Hassan Abbasi amesema mapato yatokanayo na huduma za maji taka na maji safi pia yameongezeka.

''Katika mamlaka mbalimbali miaka mitano iliyopita mapato kwa mwaka yaliyokuwa shilingi bilioni 176.87 sasa yameongezeka hadi zaidi ya shilingi bilioni 301 kwa mwaka,'' amesema Dkt. Hassan Abbasi.

Katika ujumbe wake wa kilele cha Siku ya Wanawake Dunia leo ambapo East Africa Television (EATV) na East Africa Radio zinamtambua Mwanamke kama Kinara katika jamii Dkt. Abbasi amesema, ''Leo ni Machi 8, Siku ya Wanawake Duniani, kwa niaba ya Serikali tunawatakia wanawake wote wa Tanzania heri ya siku hii na waendelee kufanya tafakuri juu ya mchango wao zaidi kwa taifa na dunia. Tunawapenda sana''.

Aidha ameongeza kuwa, ''Wanawake wameendelea kuvunja rekodi ya kushika nafasi kubwa za kiuongozi hapa nchini akiwemo Mama Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Tanzania, na Eng. Zena Ahmed Said ambaye kwa sasa ni mwanamke wa kwanza kuwa Katibu Mkuu Kiongozi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar''.
 

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP