
Kadi ya mchango
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya harusi hiyo wameeleza hali halisi iliyojitokeza siku ya kupanga bajeti ili wagawane majukumu ya kwenda kununua mahitaji ikiwemo vyakula na vinywaji, ndipo walipohitaji fedha hizo na hazikupatikana mpaka bwana harusi alipoingilia kati na kutoa pesa zake mfukoni.
Wakiendelea kutoa simulizi cha yaliyojiri siku hiyo ya kikao cha bajeti ,wanakamati wamelaani vikali kitendo kilichofanywa na mama huyo huku wakikiita ni mmommonyoko wa maadili ya kiafrika.
EATV ilifika nyumbani kwa wanafamilia hao kwa ajili ya kuhojiana nao kuhusu tuhuma zinazowakabili badala yake waligoma kuzungumzia suala hilo na kuanza kurusha maneno yaliyoashiria pesa hizo zimeliwa.