
Madawati
Akipokea madawati hayo Mheshimiwa Makonda ameshukuru na kutoa wito kwa wanafunzi wa Jiji la Dar es salaam kusomea masomo ya Sayansi ili kwenda na kasi ya mabadiliko ya sayansi teknolojia ya ulimwengu wa leo sanjari na ari ya serikali mpya ya kujenga uchumi wa viwanda kwa kuwa taifa bado lina uhaba wa wanafunzi, walimu na wataalam waliobobea katika fani hizo.
Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi ya elimu ya shule ya Al Muntazir Imitiaz Lalji amebainisha kuwa siku za karibuni limetokea kundi la wazazi wachache wanaojiita ni umoja wa wazazi wenye watoto katika shule za Almuntazir na kujaribu kuchafua jina la shule kwa kuchapisha kusambaza maaandishi ya kichochezi kwa umma.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Jumuiya ya KSIJ na Msimamizi Mkuu wa Shule za Al muntazir Bwana Azim Dweji amemuomba Mkuu wa Mkoa kuwapa eneo lenye ukubwa wa nusu hekari kwa ajili ya ujenzi wa shule nyingine kama hatua ya upanuzi wa utoaji huduma za elimu za shule za Almuntazir.