Mwenyekiti CHADEMA, Freeman Mbowe
Akitoa uamuzi huo mahakamani leo Alhamisi Machi 7, Jaji Sam Rumanyika, amesema Mahakama imeikubali rufani hiyo kama ilivyo hivyo warufani wanatakiwa wawe nje na kwamba uamuzi wa kuwafutia dhamana ulifanyika mapema mno (pre mature).
“Aidha, sharti la kuripoti polisi kila alhamisi limefutwa badala yake watariporti mahakamani mara moja kwa mwezi si polisi tena kama ilivyoamriwa na Mahakama ya Kisutu mara ya kwanza,” amesema.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliwafutiwa Mbowe na Matiko dhamana kwa madai ya kukiuka masharti ya dhamana hiyo ambapo walikata rufaa Mahakama Kuu Desemba mwaka jana na uamuzi kutolewa leo.
Walifutiwa dhamana hiyo na aliyekuwa Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri Novemba 23, 2018 lakini siku hiyohiyo kupitia kwa wakili wao Peter Kibatala walikata rufaa Mahakama Kuu chini ya hati ya dharura sana wakipinga uamuzi huo.
