Jumatatu , 4th Jul , 2016

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni amesema kuwa wilaya yake imeshakamilisha kwa asilimia 100 tatizo la Madawati lakini bado kuna changamoto ya vyumba vya madarasa ambavyo wameweka mkakati wa kumaliza tatizo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ali Salum Hapi

Akizungumza leo kwenye Hafla ya kuapishwa kwa wakuu wa Wilaya za Dar es Salaam, Mkuu huyo wa Wilaya Bw. Ali Salum Hapi amesema kuwa suala hilo licha ya kutaka msaada kutoka serikalini lakini na wadau washiriki ili kuweka mazingiria mazuri kwa wanafunzi wa wilaya kupata elimu bora.

Bw. Hapi amesema wameamua kwenda mbali zaidi katika kuweka mazingira safi ya Elimu katika wilaya hiyo ili iwe ya kupigiwa mfano kwa wilaya zote ambayo itakua na mazingira mazuri ya katika utoaji elimu kupitia sera ya Elimu bure.

Katika hatua nyingine amezungumzia mikakati ya utunzaji wa mazingira katika wilaya yake ambapo amesema kila mfanyabishara katika wilaya hiyo aweke na kifaa cha kutunzia uchafu katika maeneo yake ya biashara ili kupunguza tatizo la kuzagaa kwa taka.