Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye,
Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 12, 2022, jijini Mwanza, alipohudhuria zoezi la kuagwa kwa miili ya wanahabari, waliopoteza maisha hapo jana mkoani Simiyu, katika ajali ya gari lililokuwa katika msafara wa viongozi wa mkoa wa Mwanza waliokuwa wakielekea Ukerewe kwenye ukaguzi wa miradi.
"Tupitie ajali zote zilizohusisha wanahabari kwenye misafara, viongozi wangu wameniagiza tuwaombe wenzetu wa jeshi la polisi watuletee ripoti za ajali hizi, tuzipitie tuone kwanini zinagusa wanahabari na tuchukue hatua ya kuwalinda wanapotimiza wajibu wao kwenye misafara ya viongozi wetu," amesema Waziri Nape