Mkurugenzi mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi
Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo umetolewa hii leo Juni 6, 2022, na kueleza kuwa vipindi vya upepo mkali na mawimbi makubwa vinatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi, katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani, Tanga, visiwa Mafia, Dar es Salaam na visiwa vya Unguja na Pemba.

