
Akiongea na waandishi wa habari Kaimu Mtendaji Mkuu wa TMAA Mhandisi Gilay Shamika amesema kuwa kuna wachimbaji na wafanyabiashara ambao si waaminifu ambao huamua kupeleka madini nje ya Tanzania bila ya kufuata sheria zinazotakiwa.
Aidha amebainisha kuwa katika kesi hizo 98 madini ya Tanzanite yameonekana kutoroshwa zaidi kulikoa aina nyingine ya madini hivyo wakala unaongeza nguvu katika kuhakikisha ulinzi unakuwepo maeneo ya uwanja wa ndege na mipakani kwa ujumla.
