Kuanzia mwezi Oktoba mwaka huu , Namibia itapunguza gharama za mawasiliano kwa silimia 50 , ambapo kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya mawasiliano nchini Namibia , Emilia Nghikembua amesema kuwa moja ya gharama kubwa za mawasiliano ni kupiga simu kutoka mtandao mmoja kwenda mwingine , na kwamba punguzo hilo limenuia kuongeza ushindani zaidi.
Ameongeza kwamba kwa sasa wateja wanaweza wasione tija ya punguzo hilo, lakini tija hiyo itaonekana pale ambapo ushindani utaanza kuwa mkubwa haswa kwa makampuni ya simu kupunguza viwango vya gharama.
Mamlaka ya mawasiliano nchini Kenya mwezi uliopita ilipunguza gharama za mawasiliano kutoka shilingi za Kenya 0.99 (sawa na shilingi za Kitanzania kufikia Ksh 0.58 (Tsh. 11.6)
Nigeria na Afrika Kusini na zenyewe zimekua na mipango ya kupunguza gharama za mwasiliano ya simu.