Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Halima Mdee alianzisha tena

Jumanne , 13th Feb , 2018

Mbunge wa jimbo la Kawe (CHADEMA) Mhe. Halima Mdee amefunguka na kudai katika uchaguzi huu wa marudio unaotarajiwa kufanyika Jumamosi (Februari 17) anataka haki itendeke kwa wagombea ili amani na utulivu wa nchi uendelee kuwepo.

Mdee ametoa kauli hiyo akiwa anamuombea ridhaa mgombea wao wa jimbo la Kinondoni Salum Mwalimu ili aweze kuwa muwakilishi wa wananchi hao na kusema safarii hawatakubali kuona dhuluma ikiendelea kutendeka za kuiba kura za mgombea fulani na kwenda kwengine kama walivyozoelea kuwafanyia.

"Huu uchaguzi tunataka watawala wajue kwamba kila mbinu wanayoifanya tunaijua lakini hakuna marefu yasiyokuwa na ncha. Tunataka Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Taifa (NEC), Polisi pamoja na wasimamizi wa uchaguzi ambao watakaotumwa na CCM wajue iwe jua, mvua, matope au mchanga, tunahitaji mwenye haki yake apewe", amesema Mdee.

Pamoja na hayo, Mdee ameendelea kwa kusema "Maulid Mtulia akishinda apewe Mtulia, Salum Mwalimu akishinda apewe Salum Mwalimu. Wananchi tumechoka kufikilia kuja hapa, wananchi tumechoka kufanywa mazuzu wakati tunajielewa.Tunataka mfumo wa demokrasia uwaachiliwe ili amani na utulivu wa nchi yetu ipate kubaki kwa sababu ikivunjwa haitabaki na hakuna mtu atakayepona".

Kwa upande mwingine, Halima Mdee amesema katika nchi zilizoendelea kidemokrasia huwa hakuna vyama vinavyotawala milele wala kuwadanganya wananchi.

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji