
Kamanda wa Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es Salaam, ACP Muliro Jumanne Muliro.
Ajali hiyo iliyotokea leo Agosti 9, 2021, majira ya saa 11:15 alfajiri, ambapo gari yenye namba za usajili T 274 CBX liliwagonga wanfunzi waliofahamika kwa majina ya Collins Obed Ngowi (15) Mwanafunzi wa kidato cha pili shule ya Sekondari Makongo na Salvina Odoro Otieno Mwanafunzi wa darasa saba Shule ya Msingi Mount Sery wote wawili walifariki dunia, huku mwanafunzi Ashura wa kidato cha tano shule ya Sekondari Al-haramain akipata majeraha sehemu za mwili na alikimbizwa hospitalini.
Jeshi la Polisi limeeleza kuwa dereva huyo alikimbia mara baada ya tukio kutokea hivyo kumtaka ajisalimishe kwani hana uwezo wa kujificha zaidi ya muda wa saa 48.
Hata hivyo chanzo cha ajali hiyo bado kinachunguzwa ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa gari hilo lililohusika katika ajali.