Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

CCM yatoa agizo kwa watendaji wa serikali

Alhamisi , 22nd Aug , 2019

Watendaji wa serikali wametakiwa kutokuwa vikwazo katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali, ikiwemo miradi ya maji na barabara.

Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Ruvuma Odo Mwisho na kulia ni Katibu mkuu wizara ya Maji, Prof. Kitila Mkumbo.

Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Ruvuma Odo Mwisho, akiwa na kamati ya siasa ya mkoa kwenye ziara ya ufuatiliaji wa miradi inayotekelezwa na serikali katika wilaya ya Songea mkoani humo.

''Wizara yetu ya Maji imefikia mahala imebweteka sana, serikali inaweza kutenga fedha lakini mpaka mkandarasi azipate fedha hizo inachukua muda, inabidi tukutane na RAS ili atuambie wao kama mkoa tatizo lipo wapi kwasababu jukumu lao ni kuhimiza wizara ilete fedha hizo'', amesema Odo.

Aidha Mwenyekiti huyo, amewataka watendaji wa serikali katika ngazi zote wahakikishe wanasaidia chama hicho kutimizia ahadi zake kwa wananchi ili wasione kama wanadanganywa na serikali yao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Polilety Mgema, ameuelezea mradi huo wa maji kuwa ni mradi ambao ulianza kutekelezwa muda mrefu na wakandarasi waliondoka eneo la mradi kwa kukosa malipo hata kabla ya awamu ya tano kuingia madarakani.

Mradi huo upo katika kijiji cha Maweso halmashauri ya Madaba Wilayani Songea mkoani Ruvuma.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke