Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bango moja kuondoka na Mkurugenzi/Mkuu wa Wilaya

Jumanne , 6th Apr , 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amekemea tabia ya viongozi wa ngazi za chini kushindwa kutatua kero za wananchi hadi viongozi wa juu watembelee maeneo yao na kukutana na kero ambazo zingeweza kumalizwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia), kushoto ni moja ya bango lenye kero.

Rais Samia ameeleza hilo leo Aprili 6, 2021 Ikulu jijini Dar es salaam wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali aliowateuwa Aprili 4, 2021 ambapo amewataka kwenda kushughulikia kero za watanzania.

“Tumezoea tukienda kwenye ziara tunapokewa na mabango ambayo mengi sio ya kushughulikiwa  na viongozi wa juu, naomba bango litakaloonekana wakati viongozi wakuu wakiwa kwenye ziara yawe ni matatizo ya kitaifa, endapo tukikuta kero ndogondogo basi bango moja Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya umwekwenda,” amesema Rais Samia.

Ameongeza kuwa “Nataka niseme bango moja Mkurugenzi au Mkuu wa Wilaya mmoja amekwenda, na hii haina maana mkazuie watu wakaandike kero zao, maana najua tunapokuja watu wanakuja na mabango mbio mbio mnakwenda kuyakusanya na kuwanyuka watu ili wasiseme yanayowasibu”.

Mbali na hilo Rais Samia amewataka watendaji wa Wizara ya Ardhi kuhakikisha wanatatua migogoro ya ardhi.

“Upande wa Ardhi, watu wameporwa sana ardhi zao na wanaohusika kwenye uporaji ni watendaji wa taasisi wanahusika kutengenezea wezi nyaraka feki, acheni mara moja naomba hili likafanyiwe kazi,” - amesema Rais Samia Suluhu.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja