Jumatano , 4th Mar , 2020

Mchungaji Ambilikile Mwaisapile maarufu kama Babu wa Loliondo, amedai kuwa Mungu amemuonesha utabiri mwingine kwamba, litatokea tetemeko kubwa la ardhi muda wowote na sehemu yoyote duniani, na litadumu kwa masaa manne, lakini halitoweza kuleta madhara yoyote.

Mchungaji Ambilikile Mwaisapile maarufu Babu wa Loliondo

Babu wa Loliondo ameyabainisha hayo wakati akizungumza na EATV, na kusema kuwa licha ya idadi ya watu wanaofika kijijini hapo kupungua kwa ajili ya kunywa kikombe chake, lakini huduma yake bado inaendelea.

"Nimeelezwa na Mungu habari ya tetemeko kubwa, ambalo linakuja na halina madhara, hakuna mtu atakayekufa wala nyumba kuanguka, hata likija usiku mvua inanyesha watu wasikimbie kwenda nje litatikisa masaa manne, kuanzi saa 6:00 na litakata saa 10:00 usiku" amesema Babu wa Loliondo.

Hadi sasa ni takribani miaka tisa imepita, tangu Babu wa Loliondo alipoibua kikombe ambacho kilielezwa, kuponya magonjwa mbalimbali na kiliwavuta watu wengi kutoka nchi mbalimbali.