Lowassa akiwa a baadhi ya madiwani Halmashauri ya Magu
Fursa ambayo kiongozi huyo ameipata ni kutembelewa na madiwani kutoka Halmashauri ya Magu mkoani Mwanza ambao walifika ofisini kwake Mikocheni Dar es salaam kwa ajili ya kumuomba kutembelea halmashauri hiyo.
Wakizungumza mbele ya kiongozi huyo, Madiwani walimuomba Lowassa kutembelea Jiji la Mwanza baada ya uamuzi wake wa kurejea chama tawala ikiwa pamoja na kuhamasisha hali ya ukusanyaji wa mapato kwenye jiji hilo.
Wakati akipokelewa na uongozi mkuu wa CCM, Marchi 1, 2019 Lowassa mwenyewe hakubainisha nini sababu ya kurejea CCM, bali aliishia kusema kuwa amerudi nyumbani.
