
Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuelekea siku ya maadhimisho ya Selimundu inayoadhimishwa tarehe 17 mwezi Juni mwaka huu, Dk. Soka amesema kuna haja ya kuhamasisha watu kupima afya zao kabla ya kuamua kupata watoto kwani tatizo hilo litaongezeka zaidi katika jamii.
Aidha, Dkt. Soka ametoa wito kwa serikali kuangalia jinsi ya kuharakisha kupima vipimo kwa Watanzania ili wananchi waweze kujua afya zao na kufanya maamuzi kabla ya kuanzisha familia
