Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Akijichanganya tunachapa"- Msukuma

Jumanne , 13th Feb , 2018

Mbunge na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Msukuma amefunguka na kudai upinzani wa kweli upo ndani ya CCM na wala sio kata vyama vingine kwa maana Waziri yeyote akifanya ndio sivyo wana uwezo wa kumuadabisha.

Msukuma ametoa kauli hiyo mbele ya wananchi wa jiji la Dar es Salaam eneo la Kigogo wakati akimuombea ridhaa mgombea wao Maulid Mtulia ili aweze kupigiwa kura za ndio kwa wingi mnamo Februari 17 mwaka 2018 ambapo uchaguzi wa marudio utafanyika katika Jimbo la Kinondoni pamoja na Siha.

"Leo kuna machinga yeyote ambaye ananyanyaswa Dar es Salaam si hakuna na imetolewa amri sasa waliokamatwa na bodaboda na Polisi waachiwe lakini hawa jamaa wanasema CCM ni mbaya. Wanataka Magufuli akalale na wake zao ndio waone CCM ni nzuri",amesema Msukuma.

Pamoja na hayo, Msukuma ameendelea kwa kusema "upinzani wa kweli upo CCM ndio maana mnaona sisi Waziri yeyote akijichanganya tunachapa na tunamwambia Rais kuwa huyu hafai anatoka. Mimi nimefanya kazi na Lowassa mwaka 2015 nilikuwa nazunguka nae kwenye 'helkopta' yake".

Kwa upande mwingine, Msukuma aliwataka wananchi hao endapo Mhe. Freeman Mbowe atakanyaga eneo hilo basi wamuulize zile pesa alizouza chama cha CHADEMA amezipeleka wapi kwa madai ameshindwa hata kujenga ofisi ya chama katika eneo hilo la Kigogo.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa