Jumatano , 15th Feb , 2023

Serikali kupitia Naibu Katibu Mkuu Uwekezaji, viwanda na Biashara, Ally Gugu, imewataka wadau kuhakikisha wanamsaidia Rais Samia katika ajenda ya soko la pamoja Afrika ambalo limelenga zaidi wanawake na vijana.

Naibu Katibu Mkuu Uwekezaji, viwanda na Biashara, Ally Gugu

Hayo yanabainishwa wakati Tanzania ikiwa tayari imeanza mchakato wa kufanya biashara katika soko la pamoja  Afrika chini ya mpango wa biashara huria katika eneo huru la biashara Afrika 

Kwa upande wao wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka jumuiya ya wafanyabiashara wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na sekta binafsi wameomba mpango huo kuwanufaisha zaidi wafanyabiashara kwani sekta binafsi kwani  ndio inamchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi Afrika.

Kwa upande wa mwakilishi wa mwenyekiti wa Baraza la Biashara  Afrika Mashariki, Raphael Maganga ambaye ni Balozi wa EABC anasema Tanzania ina uwezo mkubwa wa kuuza nje bidhaa ndani ya  nchi bara la Afrika.

"Mauzo ya Tanzania barani Afrika yalifikia dola bilioni 2.5 mwaka 2021 ikiongezeka kwa asilimia 13 kutoka mwaka 2020 huku uagizaji wa bidhaa kutoka nje ukifikia dola bilioni 1.2" amesema Maganga 

Naye mshauri wa sera ya uchumi kuhusu soko huru la biashara Afrika ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Lamech Wesonga, ameitaka sekta binafsi kuchukua jukumu la kufanya biashara chini ya AfCFTA ili kufungua fursa takribani bilioni 1.3 zilizopo katika soko hilo.