Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali kuwekeza zaidi kwenye kilimo na mifugo

Jumatatu , 8th Aug , 2022

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Jenifa Omolo, amesema kuwa Serikali imeongeza bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa Mwaka wa Fedha 2022/23 kutoka Sh. bilioni 294 hadi Sh. bilioni 954 ili kuwezesha sekta ya kilimo kuwa na tija kwa Taifa.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Jenifa Omolo, akifafanua mipango ya Serikali katika kuboresha sekta ya kilimo na utayari wa Wizara ya Fedha na Mipango kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Kilimo kufanikisha utekelezaji wa mipango hiyo, alipotembelea Banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa Uwanja wa John Mwakangale, jijini Mbeya

Bi. Omolo alisema hayo alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zilizo chini yake katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa katika Uwanja wa John Mwakangale, jijini Mbeya.

Alisema kuwa lengo la kuongeza bajeti ni kuwezesha upatikanaji wa mbegu bora, kuimarisha upatikanaji wa pembejeo, utoaji wa elimu kwa wakulima kupitia kwa maafisa ugani, kujenga skimu za umwagiliaji pamoja na kujenga maeneo ya kuhifadhi mazao.


‘Katika bajeti hii ya 2022/2023 Serikali imewekeza fedha nyingi kuhakikisha kuwa kilimo kinatanuka na watu wanapata ajira kwa kuwa asilimia 70 ya Watanzania wanategemea kilimo ambacho ni uti wa mgongo,’ alisema Bi. Omolo.

Alisema kuwa Serikali  imetenga Sh. bilioni 361 ili kuwezekeza katika skimu za umwagiliaji ili kuwezesha wakulima kuendelea na shughuli za kilimo mwaka mzima bila kutegemea mvua za msimu na kiasi cha Sh. bilioni 14.9 kimetengwa kwa ajili ya mafunzo kupitia kwa maafisa ugani ili wakulima waweze kulima kisasa
 

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji