
Katika tukio hilo wafanyakazi wanne waliokuwa wakifanya kazi ndani ya ghala hilo wamejeruhiwa na moto na kukimbizwa hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya matibabu
Msemaji wa kiwanda cha Jielong Qir Fengzhou amesema moto huo ulianza kuwaka kidogo majira ya saa 11 jioni jana na wakaanza kuuzima lakini ghafula ulilipuka na kuwa mkubwa na kuomba msaada Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Shinyanga ambao walifika mapema kwa kushirikiana na magari mengine ya makampuni na kuanza kuzima moto huo kabla ya kusababisha madhara makubwa upande wa mbegu.
Mrakibu wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Shinyanga Ramadhan Kano akiwa eneo la tukio,amesema wamefanya jitihada kubwa kuzima moto huo kutokana na kuwa mkubwa na kufanikiwa kuudhibiti kabla ya kusababisha madhara makubwa upande wa mbegu.