Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mama Lishe waongezewa thamani Jijini Dar

Jumatatu , 28th Sep , 2020

East Africa Radio kwa kushirikiana na duka kubwa la bidhaa la Jaden Home Store kupitia kipindi cha Mama Mia leo wameanza rasmi zoezi la kuwaongezea thamani Mama lishe bora Jijini Dar es Salaam kwa kuwapatia zawadi ya bidhaa mbalimbali zitakazowaongeza thamani kwenye biashara zao.

Moja kati ya wamiliki wa Jaden Home Store Jacqueline Maadili (kushoto) akimkabidhi TV ya kisasa mama lishe Yolanda Paul anayeuza chakula na vinywaji Ubungo Msewe ambayo itakakwenda kuongeza thamani katika biashara yake.

Mama lishe wa kwanza kabisa kuongezewa thamani kupitia mchakato huo East Africa Radio ni Yolanda Paul wa Divine Fast Food, iliyopo Ubungo Msewe, ambaye kutokana na mahitaji yake, amepatiwa Smart TV mpya kabisa ya kisasa kutoka Jaden Home Store ambapo anaeleza kuwa TV hiyo itasaidia kuwahabarisha pamoja na kuburudisha wateja wake wakati wakipata mlo.

Nilikuwa nahitaji kitu cha kuwavutia zaidi wateja wangu wanapo kula ili kuburudika, hivyo basi nikaona iwapo nitapata TV wateja wangu wataburudika wakati wa kipata mlo jambo ambalo litazidi kuniongezea wateja zaidi,” alisema Mama lishe Yolanda huku akishukuru.

Mama lishe wa pili kuongezewa thamani kupitia mchakato huu ni Sarah Moshi wa Mwenge Jijini Dar es Salaam, ambaye kutokana na mahitaji yake, amepatiwa Blender mpya kabisa ya kisasa kutoka Jaden Home Store ambaye anaelezea furaha yake kwa kuahidi kuitumia kutengeneza juisi safi itakayoongeza thamani kwenye biashara yake.

Sarah Moshi ni Mama Lishe kutoka Mwenge Jijini Dar es Salaam , akikabidhiwa Brenda mpya kabisa ya kisasa kutoka Jaden Home Store.

Moja kati ya wamiliki wa Jaden Home Store Jacqueline Maadili akikabidhi vifaa hivyo kwa Mama Lishe hao amewasihi kukuza biashara zao kwa kuwa wabunifu na kutokata tamaa kwa kuwa maisha ni mapambano.

"Ukimsaidia mwanamke mmoja umeisaidia jamii nzima, hicho ndicho kitu kilichotuhamasisha sisi Jaden Home Store kuungana na East Africa Radio kupitia kipindi cha Mama Mia ili kuongezea thamani Mama Lishe hawa,” alisema Jacqueline.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa