Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bodi ya ushauri GPSA yahimizwa ubunifu

Ijumaa , 17th Jun , 2022

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Jenifa Omolo, ameitaka Bodi Mpya ya Ushauri ya Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) kuisimamia ipasavyo Taasisi

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Jenifa Omolo

Amesema usimamizi huo utasaidia kuongeza ubunifu na ufanisi katika kuihudumia Serikali kwenye ununuzi wa magari, mafuta na Kugomboa na kuondosha mizigo ya Serikali kutoka bandarini, viwanja vya ndege na mipakani ili kuongeza tija.

Bi. Omolo ametoa maelekezo hayo wakati akizundua Bodi mpya ya Ushauri ya Wakala huo Jijini Dar es Salaam ambapo amesema GPSA imepewa majukumu hayo na Serikali ili iweze kuihudumia lakini kuna changamoto kadhaa ambazo Wakala huo unatakiwa kuzifanyia kazi.

Alisema kuwa lengo la kuanzishwa kwa Wakala huo ni kuisaidia Serikali kupunguza gharama za uendeshaji kwa kujiendesha kwa faida lakini pia kupata huduma muhimu kama upatikanaji wa magari yanayoagizwa na wakala kwa niaba ya Serikali kwa wakati, kusogeza huduma za upatikanaji wa mafuta maeneo mbalimbali ili iweze kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Bi. Omolo ameipongeza Taasisi hiyo inayosimamiwa na Wizara ya Fedha na Mipango kwa kubuni mfumo wa utoaji mafuta ya magari ya Serikali ambao umeonesha ufanisi ambapo madereva wa Serikali wamekuwa wakipatiwa token ambazo huzitumia kujaza mafuta kwenye kituo chochote cha Mafuta cha GPSA hatua iliyoondoa usumbufu kwa madereva wa kutembea na makaratasi ya vibali.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini Dkt. Geraldine Rasheli alitoa taarifa ya utekelezaji wa kazi za GPSA na kubainisha kuwa, pamoja na mambo mengine, Wakala huo unaangalia uwezekano wa kujenga vituo vya gesi kwa ajili ya matumizi ya magari ya Serikali ikiwa ni hatua ya kukabiliana na changamoto ya upatikanaji na kupanda kwa bei za mafuta duniani.

Kwa Upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) Bi. Dorothy Mwanyika, ameihakikishia Serikali kwamba Bodi yake itasimamia utekelezaji wa maelekezo ya Serikali katika kuleta ubunifu na mikakati mipya itakayosaidia kuboresha utoaji huduma kwa wateja wake.

Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini ni kama duka la Serikali na malengo ya kuanzishwa kwake yalikuwa ni Kutoa huduma toshelevu ya vifaa/bidhaa kwa ubora na bei shindani; Kuandaa na kutoa orodha ya wazabuni wa vifaa na huduma mtambuka; Kugomboa na kuondosha mizigo ya Serikali kutoka bandarini, viwanja vya ndege na mipakani; na Kutoa huduma ya kuhifadhi mali na vifaa kwa kutumia maghala na maeneo ya wazi.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa