Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa kwanza wa Umoja wa wa vyuo vikuu vya Afrika.
Mkuu wa Mahusiano Umma na Vyombo vya Habari wa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, Annette Kanora (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu makubaliano ya ushirikiano baina ya taasisi hiyo na Benki ya NBC yanayolenga kufanikisha maandalizi ya msimu wa tano wa mbio za NBC Dodoma Marathon. Mbio hizo zenye hadhi ya kimataifa zinatarajiwa kufanyika Julai 28, mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma. Hafla ya makubaliano hayo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Mkuu wa Mahusiano ya Umma ya Umma na Mawasiliano wa NBC, Godwin Semunyu