Yanga kuwawekea kambi Ulaya, Waalgeria
Mabingwa wa ligi kuu ya soka Tanzania bara timu ya soka ya Yanga itaweka kambi nchini Uturuki kabla ya kwenda nchini Algeria kumenyana na MO Bejaia katika mchezo wa kwanza wa Kundi A Kombe la Shirikisho Barani Afrika utakaopigwa Juni 17, mwaka huu.