Halmashauri zaagizwa kujenga vyumba vya upasuaji
Serikali imezitaka halmashauri nchini kujenga vyumba vya upasuaji na maabara katika vituo vya afya ili iweze kupeleka wahudumu wengi wa afya katika maeneo yao ili kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto vinavyotokea wakati wa kujifungua.