Yafahamu haya mabadiliko ya Kombe la Dunia
Zimebaki siku 6 kabla ya fainali za Kombe la Dunia 2018 kuanza huko nchini Urusi, ambapo kipenga cha kwanza kitapulizwa Alhamisi ya Juni 14 saa 12 jioni kwa saa za Afrika Mashariki, pale wenyeji Urusi watakapokipiga na Saudi Arabia.