Sadaka ya Makonda, watoto zaidi ya 200 kunufaika
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda leo amejitolea kadi 220 za Bima ya Afya zenye thamani ya zaidi ya shilingi Million 11 kwa watoto yatima na waishio Kwenye mazingira magumu ili wapate uhakika wa matibabu mwaka mzima ikiwa ni sehemu sadaka kwa Mwezi mtukufu wa Ramadhani.