Skye ameshinda pambano la Kihistoria Saudi Arabia

Bondia wa Australia amefanikiwa kutetea ubingwa wake wa WBC uzito wa Unyoya baada ya kupata ushindi wa pointi kutoka kwa Majaji walioshuhudia pambano hilo. Pambano la kwanza la ubingwa kwa uapande wa Wanawake kufanyika nchini Saudi Arabia limetizamwa kama ni hatua chanya kwa Taifa hilo kwenye michezo kwa upande wa Wanawake na tunaweza kuanza kushuhudia Mabondia Wakike kutoka Saudi Arabia wakipambana ulingoni.

Raia wa Austraalia Skye Nicolson amefanikiwa kutetea ubingwa wake dhidi ya Raia wa Uingereza Raven Chapman kwa pointi katika pambano lililopigwa kwenye uwanja wa Kingdom Arena nchini Saudi Arabia katika Jiji la Riyadh.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS