Saturday , 4th Oct , 2025

Baada ya tetesi kusambaa kwamba Instagram hupeleleza mazungumzo ya watumiaji wake ili kuwaletea matangazo yanayohusiana na kile wanachoongea, CEO wa Instagram, Adam Mosseri, ameibuka na kukanusha vikali madai hayo.

- Ikiwa kama ni kweli tunasikiliza mazungumzo yako basi tutakuwa tunakiuka haki ya faragha kwa watumiaji wetu

- Betri ya simu yako ingekuwa inaisha kwa haraka kwa sababu microphone ingekuwa inafanya kazi muda wote.

Na kama huamini kwenye haya mawili Adam anaongeza ufafanuzi kwa kusema:

- Ukiona Tangazo umeliona kwenye timeline yako basi fahamu fika ni moja ya kitu ambacho umekuwa ukikitafuta kwa ukaribu kwenye mtandao huo.

- Instagram hushirikiana na watangazaji (advertisers) wanaolipia kufikia watu wenye Kundi au uhitaji wa kitu fulani, na siyo kwa kusikiliza mazungumzo binafsi.

Kwa kifupi: Instagram haikusikilizi, bali inakuonyesha kile unachokihitaji mtandaoni.