
Theonas Mwinuka maarufu kama Razack
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Tumaini Maleko, kufuatia ushahidi thabiti uliowasilishwa na upande wa mashtaka ukiongozwa na mawakili wa serikali Majid Matitu na Kashindye Maganga.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, Mwinuka alitenda kosa hilo la kikatili katika kijiji cha Ruaha Mbuyuni, ambapo alitumia nguvu na kusababisha majeraha makubwa kwa mtoto huyo kabla ya kumtupa mtoni kwa lengo la kuficha ushahidi.
Hakimu Maleko alieleza kuwa mahakama imezingatia ushahidi wa muhanga, mlezi wake, daktari na maelezo ya mshtakiwa, na kuthibitisha kosa hilo pasipo shaka yoyote.
Mwinuka amehukumiwa chini ya Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 (Marejeo ya mwaka 2022), Kifungu cha 130(1)(2) pamoja na Kifungu cha 131(3), vinavyohusiana na makosa ya ubakaji kwa watoto.
Mahakama imesisitiza kuwa hukumu hiyo iwe fundisho kwa watu wote wanaojihusisha na vitendo vya kikatili dhidi ya watoto, ikieleza kuwa haki za mtoto ni za msingi na zinapaswa kulindwa kwa nguvu zote za kisheria.