Friday , 7th Mar , 2025

Jeshi la Polisi mkoa wa Tanga linamshikilia kwa mahojiano bondia Hassan Mwakinyo, kwa tuhuma za kumshambulia mtu anayedaiwa kuingia katika eneo lake bila ya ridhaa yake.

Bondia Hassan Mwakinyo

Mwakinyo anashikiliwa tangu jana Machi 6, 2025, huku mtu aliyemshambulia akiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo Tanga.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga ameeleza kuwa mtu huyo anayedaiwa kushambuliwa na Mwakinyo, inadaiwa alipita maeneo ya nyumbani kwake na kutaka kuingia katika mazingira yanayodaiwa kuwa na nia ya kutenda kosa na ndipo alipomkamata na polisi walipofika eneo la tukio walimkuta mtu huyo ana majeraha kidogo.