Friday , 13th Sep , 2024

Mchezaji wa klabu ya Manchester city Erling Halland amefanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi wa ligi kuu Uingereza baada ya kuwa na mwendelezo mzuri wa kiwango kwenye michezo ya timu yake katika mwezi huo.

Aidha mkufunzi wa klabu ya Brighton Fabian Hurzeler amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi baada ya kuiwezesha klabu yake kupata alama 7 katika michezo mitatu ya kwanza ndani ya klabu hiyo.