Sunday , 11th Aug , 2024

Jeshi la polisi nchini limepiga marufuku maandamano au mikusanyiko ya aina yoyote ile inayotaka kufanyika kwa mwavuli wa kuadhimisha siku ya vijana duniani kwa mkoa wa Mbeya kwasababu yamelenga kuvunja amani na utulivu wa taifa

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Tanzania, Awadhi Juma Haji

Hayo yamebainishwa na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Tanzania, Awadhi Juma Haji ambaye amesema jeshi la polisi litaendelea kupambana na viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani ikiwemo maandamano hayo ambayo yamelenga kuvuruga amani

Amewaagiza makamanda wa Polisi wa Mikoa (RPC) kufanya ukaguzi kwenye mabasi yanayoelekea jijini Mbeya kwenye kongamano la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kuwachukua hatua wahusika.

Haji ametoa maagizo hayo leo Jumapili, Agosti 11, 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Mbeya ikiwa kufuatia uwepo wa taarifa za kongamano hilo lililopangwa kufanyika kesho Jumatatu, Agosti 12, 2024, Viwanja vya Ruanda Nzomve kupigwa marufuku na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.