Monday , 29th Jul , 2024

Mabehewa matano kati ya 20 yaliyokuwa yamebeba mzigo wa ngano kutoka Dar es Salaam kwenda Isaka yameanguka leo Julai 29, 2024 katika eneo la Bigwa Sista Manispaa ya Morogoro mkoani humo.

Moja ya behewa lililoanguka

Kwa mujibu wa Stesheni Masta Msaidizi Godfrey Temba ajali hiyo imetokea leo majira ya saa 12 jioni na kwamba hakuna madhara kwa upande wa binadamu.

Aidha hadi sasa sababu za mabehewa hayo kuanguka hazijatajwa.