Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Miradi mikubwa 9 ya kimkakati kutekelezwa Songwe

Friday , 22nd Mar , 2024

Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imekusudia kutekeleza miradi mikubwa 9 ya kimkakati ikiwemo upanuzi wa barabara kuu ya TANZAM kipande cha Igawa – Tunduma (km 218) na Ujenzi wa kituo cha ukaguzi wa pamoja wa magari katika barabara hiyo eneo la Iboya Songwe.

Meneja wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Songwe Suleiman Bishanga amesema hayo tarehe 19 Machi 2024; alipozungumza na Kipindi cha TANROADS Mkoa kwa Mkoa kuhusu mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita katika sekta ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja.

Amemtaja mkandarasi anayejenga barabara hiyo ya njia nne kwa utaratibu wa EPC + F ni M/s China Civil and Engineering Construction Coopration (CCECC) kutoka China; ambaye tayari ameshaanza maandalizi ya kuainisha maeneo ya kujenga kambi.

Amesema pia mradi huo utakuwa na barabara za mchepuo (Bypass) ili kuondoa msongamano wa magari hasa malori katikati ya mji.

Amesema miradi mingine ambayo ipo kwenye mipango ya Serikali katika ujenzi ni Barabara ya Mlowo – Kamsamba na Spur Road ya Chitete Makao Makuu ya Wilaya ya Momba (Km 147) na tayari imeshakamilisha ujenzi wa daraja la Momba linalounganisha Mkoa wa Songwe na Rukwa. 

Pia Barabara ya Isongole II – Ngana / Mbeya – Kasumulu hadi Katumbosongwe Km 124). Sehemu ya Kwanza ya Isongole II – Ibungu – Isoko (Km 52.419) ujenzi unatarajia kuanza hivi karibuni kwani zabuni ilishatangazwa na kumpata mkandarasi wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara hiyo na ulipaji wa fidia wa mali, nyumba na mazao umeshakamilika ambapo waathiriwa wa mradi wapatao 312 wamelipwa fidia ya jumla ya TZS Milioni 850.269.

Barabara ya Ruanda – Nyimbili – Izilya – Itumba (Km 79) na Mahenje – Haasamba – Vwawa Km 32. Sehemu ya kwanza km 1.2 Mkandarasi aitwae GNMS Contractors C. Ltd kutoka Iringa anaendelea na kazi; sehemu iliyobaki ya Ruanda – Idiwili km 20 imetengwa sehemu nne za km 5 kila moja ambapo ujenzi wa kiwango cha lami wa sehemu hiyo utafanywa na Wakandarasi Wanawake.

Bishanga ametaja mradi mwingine ni Barabara ya Mbalizi – Chang’ombe – Mkwajuni – Saza – Patamela hadi Makongorosi Km 110, Sehemu ya Chang’ombe – Mkwajuni – Saza – Patamela hadi Makongorosi Km 61, Barabara ya Ibungu – Kafwafwa na Itumba – Shigamba – Ibaba – Katengere pamoja na Ujenzi wa madaraja mawili ya Magamba na Namkukwe katika barabara ya Galula – Namkukwe (Km44.3).

HABARI ZAIDI

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12