Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
Kauli hiyo ameitoa hii leo jijini Dar es Salaam, mara baada ya kuwaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni, wakiwemo majaji hao pamoja na Naibu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
"Hakikisheni mnasimamia haki za watu, mwenye haki aipate, unajua suala la kutoa haki ni la Mungu peke yake, sasa kama Mungu amekujaalia umeteuliwa kusimamia haki za wanadamu wenzio unafanya kazi inayofanana hapo, kasimamieni haki sababu mmeapa na mmeshika vitabu mnavyoviamini, mtakwenda kuulizwa kwanini ulipindisha haki kwa pesa chache ambayo ukitumia hata mwezi haufiki, hata kama utajenga lijumba la fahari halafu si utakufa utaliacha, na ukiliacha watoto wako wanauza," amesema Rais Samia
Aidha akizungumzia suala la serikali kuingia mikataba mbalimbali ya uwekezaji na mataifa mengine, amemtaka Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Balozi Profesa Kennedy Gastorn, akawe mstari wa mbele kuhakikisha serikali haiingii kwenye matatizo ya kiuwekezaji.
Awali akizungumza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewapongeza walioapa hii leo kwa kupata nafasi ya kuaminiwa na Rais Samia huku matarajio yake ni kuona utendaji wenye weledi, uaminifu na uadilifu wa dhati.