Saturday , 26th Aug , 2023

Viongozi wa mapinduzi nchini Niger wamempa balozi wa Ufaransa saa 48 kuondoka nchini humo wakati uhusiano wa nchi hizo mbili ukiendelea kuzorota kwa kasi.

Paris inapinga mapinduzi ya mwezi Julai, ikisema kuwa rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Bazoum lazima arudishwe madarakani.

Serikali ya nchi hiyo imesema Sylvain Itte amekataa kujibu mwaliko wa kukutana na waziri wa mambo ya nje wa Niger.

Ufaransa, taifa la zamani la kikoloni, limesema wapiganaji wa kundi hilo hawana mamlaka ya kuamuru kufukuzwa kwa aina hiyo.

Paris inapinga mapinduzi ya mwezi Julai, ikisema kuwa rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Bazoum lazima arudishwe madarakani.

Tangazo la Ijumaa lilitolewa na waziri wa mambo ya nje wa Niger aliyewekwa na junta.Hii inafuatia mfululizo wa kauli na maandamano ya chuki dhidi ya Ufaransa.Wizara ya mambo ya nje ya Ufaransa ilijibu kwa kusema kuwa  imewachukulia hatua wale waliowashambulia, shirika la habari la AFP limeripoti.