Friday , 28th Jul , 2023

Rais wa Urusi Vladimir Putin amewaambia viongozi wa Afrika Ijumaa ya leo mjini Moscow kuwa  anaheshimu pendekezo lao la amani kuhusu Ukraine na alikuwa akilichunguza kwa makini

Putin pia ameuambia mkutano wa kilele wa Urusi na Afrika kwamba Urusi inaongeza usambazaji wa chakula kwa Afrika, ikiwa ni pamoja na usafirishaji wa nafaka bila malipo ambayo alitangaza siku moja kabla, na ina nia ya kuendeleza ushirikiano wa kijeshi na bara hilo

Viongozi wa Afrika waliwasilisha mpango wao wa amani mwezi uliopita kwa Putin na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy lakini umeshindwa kupata maelewano na pande zote mbili.