
Ruto amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter na kueleza nia yake hiyo ya kuonana na Odinga
“Rafiki yangu Raila Odinga nipo Tanzania kwa ajili ya mkutano wa Rasilimali watu ili kuoanisha upanuzi wa nafasi za ajira katika bara letu. Nitarudi kesho jioni, na kama ulivyokuwa ukijua, ninapatikana na niki tayari kwa mazungumzo ya ana kwa ana wakati wowote kwa urahisi” Anaandika Rais Ruto.
Itakumbukwa mapema leo mchana Raila Odinga alizungumza na wanahabari na kusema kuwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alienda nchini Kenya Kwa ajili ya kuwapatanisha lakini Rais Ruto alikwamisha jitihada hizo.