Mgongo ulioungua
Inaelezwa kuwa mtoto huyo alikuwa akipatiwa matibabu kwa kulazwa kwenye kitanda cha kienyeji (kitanda cha kamba) ambapo chini yake kulikuwa na moto unaochemsha maji kwenye Sufuria, maji ambayo yalitoa mvuke mkali na kumfikia mtoto huyo wa darasa la kwanza na kumuunguza eneo la mgongoni.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Lindi ACP Pili Mande, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuthibitisha kuendelea kumshikilia Jalina Liwajila (mganga wa kienyeji) kwa mahojiano zaidi