Tuesday , 27th Jun , 2023

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Pindi Chana, amewakaribisha wadau na wapenda michezo wa sekta binafsi wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika shughuli za michezo hususani mchezo wa netiboli.

Waziri Chana ameyasema hayo  Dar es Salaam wakati akifungua mashindano ya klabu bingwa ya netiboli katika Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam.

"Nimepokea taarifa ,nimetoe maelekezo kwa BMT kuhakikisha mnakaa na chama Kisha mniletee mapendekezo ," amesema Dkt Pindi .

Ametoa wito kwa wadau wengine zikiwemo taasisi kuwekeza pia katika ujenzi wa miundombinu ya kimichezo na kugharamia shughuli za michezo hususani michezo ya wanawake pamoja na watu wenye ulemavu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli (Chaneta), Dk Devota Marwa amesema kuwa wataendelea kuratibu programu mbalimbali za maendeleo ya mchezo huo.

"Pamoja na hayo badowanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mdhamini  wa kudhamini matukio mbalimbali ya Chama," amesema  Dkt Devotha.

Timu 13 shiriki ni pamoja  Tamisemi,Jeshi stars,Nyika Queens,Eagle Queens ,JKT Mgulani,JKT Mbweni ,Upendo,NSSF,Polisi Arusha,Kampala,Uhamiaji  ,Bukoba Queens na Tanroad