Monday , 5th Jun , 2023

Watu watano wamefariki dunia na wengine 20 kujeruhiwa baada ya gari aina ya Coster yenye namba za usajili iliyokuwa ikitoka Mbeya kuelekea Dar es Salaam kuligonga ubavuni Lori lenye tenki la mafuta wakati alipotaka kulivuka Lori lingine bila kuchukua tahadhari.

Coaster iliyopata ajali na kuua watano

Ajali hiyo imetolea  Alfajiri ya leo Juni 5, 2023, wakati dereva wa Coster yenye namba T 938 DVQ iliyokuwa ikitokea Mbeya kuelekea Dar-es-Salam kutaka kuyapita magari mengina na kugongana na gari aina Lori lenye tenki ya mafuta T 693 DMF -T 586 CKR iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Iringa.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro ACP Alex Mkama, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo amesema wanamtafuta dereva wa Coaster ambaye amesababisha vifo vya watu hao na majeruhi.

Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali ya St.Kizito Mikumi mkoani humo Steven Mbilinyi, amesema tayari wamepokea miili ya watu 5 wanaume 3 na wanawake 2 na majeruhi 20.